Ukosefu wa ajira na makazi salama vyawaacha wafanyakazi wahamiaji hatarini Lebanon:IOM

Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM limesema ukosefu wa ajira endelevu na makazi salama kutokana na janga la corona au COVID-19 na athari zake za kiuchumi vimewaacha maelfu ya wafanyakazi wahamiaji nchini Lebanon katrika hatari kubwa ya usafirishaji haramu wa binadamu na ukatili.


Kwa mujibu wa taarifa ya IOM iliyotolewa leo mjini Beirut, milipuko miwili iliyotokea mjini humo Agosti 4 mwaka huu imefanya hali kubwa mbaya zaidi na kufanya maelfu ya wafanyakazi wahamiaji kukosa ajira na kutokuwa na njia ya kurejea nyumbani. 

IOM inakadiria kwamba takriban wahamiaji 24,500 mjini Beirut wamepoteza kazi zao, makazi yao au kuathirika kwa njia moja au nyingine na milipuko ya Beirut. 

Swahili | October 26, 2020

COMMENTS

SUPPORT OUR WORK

We depend on your donation to fight for domestic workers in Lebanon.